Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini na aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, ametoa kauli yake rasmi muda mfupi baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutangaza Baraza jipya la Mawaziri kwa mwaka 2025–2030, ambapo jina lake halimo katika orodha ya walioteuliwa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bashe ameanza kwa kumshukuru Mungu na kuonesha shukrani kubwa kwa Rais Samia kwa imani aliyooneshwa kwake katika kipindi cha awamu ya kwanza ya uongozi wake, akimpa nafasi kwanza kama Naibu Waziri, kisha Waziri wa Kilimo. “Ni heshima niliyothamini kwa moyo wangu wote, na ninaendelea kuwa mwenye shukrani kwa nafasi hiyo ya kuwatumikia Watanzania,” ameandika. Akimpongeza Waziri mpya wa Kilimo, Daniel Chongolo, Bashe amesema anamfahamu kama “mzalendo na mkulima,” na anaamini atamsaidia Rais kutimiza matarajio ya Watanzania. Pia amempongeza Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde, akisema hana mashaka naye na anamfahamu kama “mzazi na mtu atakayekuwa msaada mkubwa...
- Get link
- X
- Other Apps